news

Zuma atuma vikosi vya jeshi kulinda bunge

Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma, ameamrisha vikosi vya kijeshi vipatavyo 440, kutoa usalama katika majengo ya bunge, wakati atakapokuwa akilihutubia taifa leo Alhamisi.

Vyama vya upinzani vimelaani hatua hiyo na kusema hiyo ni "kutangaza vita".

Hotuba za hapo awali za Bw Zuma, zilikumbwa na maandamano na fujo, huku wabunge wa upinzani wakitoa wito wa kujiuzulu kwake. Kwa muongo mmoja uliopita, Bw Zuma amekuwa akiandamwa na madai ya kashfa ya ufisadi. Zuma adaiwa kusinzia bungeni

Jacob Zuma : Siogopi kufungwa jela Zuma arudisha pesa zilizokarabati nyumba yake Zuma aepuka kura ya kutokuwa na imani naye Wanachama wa ANC waandamana dhidi ya rais Zuma Taarifa kutoka kwa Ofisi ya rais na iliyotolewa siku ya Jumanne, inasema kuwa Bw Zuma aliamrisha kutumwa kwa vikosi hivyo vya wanajeshi, ili kushirikiana na maafisa wa polisi kutoa ulinzi.

Hii ni mara ya kwanza kwa wanajeshi wa nchi hiyo, kudumisha usalama, badala ya kuhusika katika sherehe. Kwa mujibu wa taarifa zilizochapishwa katika vyombo vya habari nchini humo, duru za kiusalama zimeonya kuwa kutatokea maandamano makubwa katika hafla hiyo.

Duru hizo zilisababisha hofu, kwamba huenda polisi wakashindwa kukabiliana nayo. Hotuba za awali za kitaifa, zilikumbwa na fujo ndani ya bunge.

Tangu waliposhinda viti katika uchaguzi mkuu mwaka 2014, wanachama wa chama cha Economic Freedom Fighters (EFF), wamekuwa wakitatiza hotuba ya rais Zuma na vikao vingi vya bunge kwa kupiga kelele na kumfokea hadharani rais kuhusiana na madai hayo ya kashfa ya ufisadi.

Mnamo mwaka 2015, wanachama hao wa EFF waliondolewa katika ukumbi wa bunge na walinda usalama waliokuwa wakijifanya kama wahudumu wa Bunge. Lakini chama kikuu cha upinzani cha Democratic Alliance (DA) kimelaani vikali hatua hiyo ya Rais, na kueleza kuwa ni "ya kutamausha mno".

"Matamshi ya mara kwa mara ya Rais Zuma 'kudumisha sheria na usalama' kwenye taarifa yake, yanaashiria matumizi mabaya ya vikosi vya jeshi nje ya majukumu yao ya kuhusika katika sherehe za kitaifa ndani ya nchi," tkulingana na chama cha DA imesema.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *